Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa zawadi ya Tsh milioni 10 kwa kila goli ambalo Klabu ya Simba itafunga katika mchezo wa African Football League dhidi ya Al Ahly.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa zawadi ya Tsh milioni 10 kwa kila goli ambalo Klabu ya Simba itafunga katika mchezo wa African Football League dhidi ya Al Ahly. Michuano hiyo inayohusisha timu nane tu itaanza keshokutwa, Ijumaa, Oktoba 20, 2023 ambapo mchezo wa ufunguzi utakuwa kati ya Simba na AL Ahly majira ya saa 12:00 jioni katika Uwanja wa Mkapa.