Taarifa zinasema kuwa Winga wa Simba Sports Club, Aubin Kramo ameongeza mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kubakia kwa miaka mingine miwili, mkataba wa awali wa Aubin Kramo ulikuwa unaisha 2025 ila baada ya kuongeza mwaka mmoja sasa utaisha mwaka 2026.
Kramo ataendelea kubaki Simba SC hadi mwaka 2026.Tukio hilo limeacha maswali mengi ikizingatiwa kuwa Mchezaji huyo ametumika kwa kiasi kidogo msimu uliopita kutokana na kusumbuliwa na majeraha.
Wengi walitarajia kuwa mchezaji huyo ataoneshwa mlango wa kutokea lakini imekuwa tofauti.
Je una maoni gani kwa kitendo cha Kramo kusalia Msimbazi? atawafikisha Simba nchi ya ahadi msimu ujao? Tupe maoni yako