Tue, 24 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Winga wa kushoto Muivory Coast wa Simba SC, Aubin Kramo Kouamé amefanyiwa upasuaji wa goti katika Hospitali ya El Yosr Internationale Sousse nchini Tunisia.
Aubin Kramo Kouamé amesajiliwa msimu huu Simba SC kutoka ASEC Mimosas ya kwao, Ivory Coast lakini kutokana na kuandamwa na maumivu ameshindwa kupata fursa ya kuonyesha makali yake nchini.
Inakadiriwa kuwa mchezaji huyo atakuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: