Simba imefanya usajili wa mlinzi wa kati kutoka Cameroon Che Malone Fondoh ambae jana alianza katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Power Dynamos ya Zambia.
Usajili huo ni katika harakati za kuziba pengo la mlinzi wa kati baada ya Simba kumtoa kwa Mkopo Joash Onyango katika Klabu ya Singida FG.
Sasa mchambuzi wa michezo kutoka TV3 Alex Ngereza amemzungumzia beki huyo kwa jicho lake la kiuchambuzi ambapo amesema;
"Che malone ni wakawaida sana na nikiulizwa naweza kutoa sababu, moja hajakutana na upinzani halisi namaanisha kucheza ligi kuu lile la jana lilikuwa bonanza haliwezi kuonyesha uwezo halisi wa mchezaji wakwenda kucheza Super League"