Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Al Ahly kama Simba, Mamelodi

Kikosi Ahly.jpeg Kocha Mkuu wa Al Ahly ya Misri, Marcel Koller.

Tue, 10 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha Mkuu wa Al Ahly ya Misri, Marcel Koller, alia na mfululizo wa mechi huku akiitaja ratiba kuwa kikwazo kwa timu yake kupata matokeo mazuri hasa kwenye michuano mipya ya African Football League inayotarajiwa kuzinduliwa Dar es Salaam.

Koller ameyasema hayo siku chache kabla ya mchezo wake wa kwanza wa ufunguzi wa AFL dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa, akisistiza kuwa wachezaji wake wametumika sana hivyo anahofia wanaweza wasimpe anachokitaka kwenye mchezo huo.

Amekumbusha kuwa kwenye mazingira kama hayo walijikuta wakipoteza taji la African Super Cup.

“Ratiba zinapangwa bila kuwajali wachezaji, kwenye mazingira kama haya sijui tutarajie nini. Inajulikana kabisa ni masaa mengi kusafiri ndani ya bara la Afrika, bado itategemea wachezaji wangu watakuwa kwenye mazingira gani baada ya kutua Tanzania, hapo ndio tutajua tutacheza vipi.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: