Wakati Joto la Mechi ya watani wa Jadi Simba na Yanga, likiendelea kupanda kuelekea Novemba 5.
Ofisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally amesema kuwa kwao mechi hiyo haina ugumu wowote na wanatarajia kuchukua alama tatu kama ambavyo wamechukua katika michezo yao 6 iliyopita.
Akizungumza Ahmed Ally anasema;
"Ni mechi ambayo tunakwenda kuendeleza ubabe kwa watani zetu. Ili tujiridhishe kwamba msimu huu tutafanya vizuri ni kupata ushindi katika mchezo huo.
Tunataka tuchukue ubingwa mapema sana, katika hili tunawashukuru Ihefu kwa kutusaidia kazi na sisi tunataka kuendeleza kuweka tofauti ya alama na Yanga SC."