Wed, 9 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya mchezo wa Ngao ya Jamii, uliowakutanisha Yanga SC na Azam FC, kumalizika kwa Yanga kuipiga timu ya Azam FC goli 2-0, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba SC, Ahmed Ally ameonyesha kufurahishwa na matokeo hayo.
Kupitia ukurasa wake wa #Instagram, Ahmed ameandika ujumbe huu; "Woooow Tumeyapenda matokeo".
Ikumbukwe kuwa, kesho Simba itacheza na Singida Fountain Gate katika mchezo aa nusu fainali ya pili ya Ngao ya Jamii na mshindi waechi hiyo atakutana fainali na Yanga.
Tuambie kupitia #comment, unadhani nini kimemfanya Ahmed Ally, ayafurahie matokeo hayo?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: