Wawakilishi wa Tanzania katika Michuano ya African Football League Timu ya Simba inashuka Dimbani muda mchache kutoka sasa kuvaana na Al Ahly.
Mchezo huo wa mkondo wa pili hatua ya Robo Fainali unapigwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Cairo.
Mchezo wa Mkondo wa kwanza uliopigwa katika Uwanja wa Mkapa Jijini Dar Juma lililopita ulimazilika kwa sare ya mabao 2-2.
Simba wanahitaji ushindi au sare ya kuanzia mabao matatu kujihakikishia nafasi ya kufuzu kwa hatua ya Nusu Fainali.
Hili hapa Jeshi la Simba linaloanza mchezo wa leo;
Ally Salim
Kapombe
Zimbwe Jr
Che Malone
Inonga
Kanoute
Ngoma
Chama
Kibu D
Saido
Bocco