Thu, 29 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nawaza tu kuwa Simba SC dirisha lijalo la usajili wakiwauza Freddy, Jobe, Miquissone na Ntibazonkiza halafu pesa hiyo wakaenda kuinasa saini ya straika wa mpira Fiston Kalala Mayele ikiwa ataondoka Pyramids, nadhani litakuwa ingizo nzuri sana na?
Baada ya Mayele, wakamuongezea mkataba wa mwaka mmoja Clatous Chota Chama. Kwa uzoefu na exposure waliyonayo Simba, wakimnasa Mayele naona wakitinga fainali klabu bingwa Afrika msimu ujao.
Nafikiri Abdelhak Benchikha akipatiwa Mayele kwa basic football aliyonayo ya hatari sana kwenye mpira atawapeleka mbali Simba kimataifa. Simba wawekeze pesa na itawalipa sana.
Columnist: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: