Tue, 9 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Za ndani kabisa zinaeleza kuwa, tayari Klabu ya Yanga Sc imefika makubaliano na Ibrahim Bacca kuongeza mkataba wa miaka mitatu zaidi kuendelea kusalia Jangwani.
Ibrahim Bacca amekuwa na kiwango Bora sana tangu alipoaminiwa katika kikosi cha kwanza Cha Yanga Sc mpaka kuitwa kwa mara ya kwanza timu ya Taifa ya Tanzania.
Baada ya Yanga kutinga nusu fainali ya Kombe lka Shirikisho Afrika, Rais wa yanga, Eng. Hersi Said alisema kuwa wameanza mazungumzo na Bacca ili kuboresha maslahi yake na kumuongezea mkataba kuendelea kuwatumikia Wananchi kwa miaka mingine ijayo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: