Thu, 1 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Yanga kimeondoka katika Uwanja wa ndege wa kimataifa Julius Nyerere kuelekea Algeria kwa ajili ya mechi ya mkondo wa pili dhidi ya USM ALGER Jumamosi Juni 3, 2023.
Mechi ya kwanza ya fainalo ya Kombe la Shirikisho Afrika, Yanga ilipoteza kwa kufungwa bao 2-1 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Yanga imeondoka na Ndege ya Serikali waliyopewa na Rais Samia Saluhu ikiwa na kikosi cha wachezaji 29, benchi la ufundi na viongozi mbalimbali waandamizi wa klabu hiyo pamoja na mashabiki.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: