Kikosi chetu kimeanza safari kuelekea nchini Nigeria ambapo tutacheza mchezo wetu wa kwanza wa hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Rivers United.
Mchezo wa kwanza utachezwa saa 10:00 jioni (kwa saa za Tanzania) siku ya Jumapili, Aprili 23, 2023, kwenye dimba la Godswill Akpabio unaopatikana kwenye Jimbo la Akwa Ibom Kusini mwa Nigeria.
Kikosi kilichoondoka leo saa 12:00 alfajiri na Shirika la Ndege la Ethiopia kuelekea Nigeria kupitia Addis Ababa na tukitarajiwa kutua jijini Lagos, nchini Nigeria majira ya saa 6:30 mchana.
Orodha kamili ya wachezaji watakaosafiri ni;
Djigui Diarra
Metacha Mnata
Erick Johora
Ibrahim Bacca
Bakari Mwamnyeto
Dickson Job
Kibwana Shomari
Farid Mussa
Mudathir Yahya
Zawadi Mauya
Yanick Bangala
Jesus Moloko
Khalid Aucho
Djuma Shabani
Fiston Mayele
Kennedy Musonda
Stephane Aziz KI
Joyce Lomalisa
Tuisila Kisinda
Salum Abubakar
Mamadou Doumbia
Clement Mzize
Bernard Morrison.