Sun, 19 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabao ya Kennedy Musonda na Fiston Kalala Mayele yametosha kuipa Klabu ya Yanga ushindi wa bao 2-0 dhidi ya US Monastir ya Tunisia katika mechi ya Kundi D ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Timu hizo mbili zimefanikiwa kusonga mbele zikiwa na pointi 10 kila moja lakini Yanga ikiwa na wastani mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Mchezo mwingine wa Kundi D, TP Mazembe imefungwa magoli 2-1 na Real Bamako.
Yanga bado ina mchezo mmoja ambapo itacheza na TP Mazembe nchini Congo DR huku Monastir akimaliza na Real Bamako.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: