Klabu ya Yanga, imeingia makubaliano ya ushirikiano na timu ya Wakiso FC ya Uganda kushirikiana kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ya michezo ikiwemo baadhi ya wachezaji wao kuja Yanga SC kujifunza na kupata Uzoefu.
Klabu ya Yanga, imeingia makubaliano ya ushirikiano na timu ya Wakiso FC ya Uganda kushirikiana kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ya michezo ikiwemo baadhi ya wachezaji wao kuja Yanga SC kujifunza na kupata Uzoefu. Yanga SC imesafiri kuelekea Malawi na wachezaji wawili kutoka Wakiso FC, Moses Aliro na Shariphu Kimbowa ambao wamekuja kupata uzoefu wa mafunzo na hivyo wamesafiri na timu lakini pia watashiriki kwenye maandalizi ya msimu (PRE-SEASON) na baada ya hapo watarejea Katika timu ya Wakiso FC.