Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga yafukuzia rekodi hii

Yanga Kamwe Kd Yanga yafukuzia rekodi hii

Sun, 26 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kwa sasa mashabiki wa Yanga wana raha ya aina yake baada ya kuishuhudia timu yao ikitinga robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika

Wananchi wanaona kabisa ni msimu ambao huenda wakaenda kushuhudia kupatikana mafanikio makubwa katika klabu yao kwenye miaka ya hivi karibuni

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema baada ya kufanikiwa kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho, malengo sasa ni kuitafuta nusu fainali, fainali na hata kusaka taji la kwanza barani Afrika kwani inawezekana

Wakati bendera ya Kimataifa ikiendelea kupepea vyema, Yanga pia imedhamiria kutetea mataji yake yote ya ndani

Ngao ya Jamii tayari iko mikononi, dalili njema zinaonekana kwenye ligi kuu, Yanga ikiwa kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama nane huku zikiwa zimesalia mechi sita kuhitimisha msimu

Kimahesabu Yanga inahitaji kushinda mechi tatu zinazofuata ili kutetea ubingwa. Kama Wananchi watashinda mehci dhidi ya Kagera Sugar, Simba na Singida Big Stars basi hesabu zitakamilika mapema tu

Lakini iwapo itatokea watani zao Simba watashindwa kupata ushindi katika mechi zao zinazofuata kazi itakuwa rahisi zaidi

Kwenye kombe la FA Wananchi wako hatua ya robo fainali wakitarajiwa kuchuana na Geita Gold

Kama hesabu zitakwenda sawa, Yanga inaweza kufunga msimu ikiwa na mataji manne na kufanya msimu huu kuingia katika kumbukumbu ya klabu

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: