Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga watangaza siku ya kurudi Skudu Makudubela

Skudu Raha Winga wa Yanga, Skudu Makudubela

Thu, 24 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga, Alli Kamwe akizungumza leo na waandisi wa habari amesema kesho siku ya Ijumaa Mahlatse Makudubela 'Skudu' atarejea nchini akitokea nchini kwao Afrika Kusini alipokwenda kushughulikia hati yake ya kusafiria (passport) ambayo imejaa.

"Skudu kweli alisafiri kwenda Afrika Kusini na kesho Ijumaa atarejea nchini Kocha Gamondi akitaka kumtumia Jumamosi ni maamuzi yake , amepona kabisa na tuliwaaambia amekwenda kushugulikia passport yake ya kusafiria"

Skudu alishindwa kuendelea na mchezo katika Nusu fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Azam, baada ya kuchezewa rafu dakika ya saba na kiungo wa Azam, James Akaminko.

Na Yanga iliichapa Azam 2-0 mabao yalifungwa na Aziz KI na Clement Mzize ambayo yamefungwa katika dakika 10 za mwisho za mchezo huo.

Skudu ameweka rekodi ndani ya Yanga ya kuwa mchezaji wa kwanza raia wa Afrika Kusini kuwatumikia mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya NBC na Kombe la Shirikisho la Azam.

Mbali na Marumo staa huyo pia amewahi kuzichezea timu za Afrika Kusini, Chippa United na Orlando Pirates kwa mafanikio makubwa, anatajwa kuwa mmoja kati ya wachezaji wenye uzoefu sana kwenye Ligi Kuu Afrika Kusini.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: