Ni ukweli usiopingika, soka la Tanzania limekuwa kivutio kwa nyota wa kigeni tangu miaka ya 1970 hadi leo, ikishuhudiwa mastaa mbalimbali kutoka mataifa tofauti wakimiminika kuja kucheza nchini.
Rekodi zinaonyesha, Hafiz Wontah Konkoni anakuwa mchezaji wa Saba (7) kutoka Ghana kuichezea Yanga kwa miaka ya hivi karibuni baada ya kipa Yew Berko, washambuliaji Issack Boakye, Kenneth Asamoah na Michael Sarpong, mbali na viungo Ernest Boakye na Bernard Morrison aliyetemwa msimu uliopita.
Wananchi kwa idadi ya hao waliotajwa unadhani Mghana yupi alifanya vyema katika Klabu ya Yanga? Tupe maoni yako