Siku zote nasemaga Tofauti ya wachezaji wa timu kubwa na ndogo ni "ubongo"
Ili tukutambue kama mchezaji wa daraja la juu tutapima zaidi ubongo wako,jinsi gani unafanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi.
That man Pacome Zouzoua ni ubongo mtupu
Tazama mikimbio yake shimoni kama namba 10 muda wote yuko Sharp,ana-scan nafasi kabla ya kupokea mpira hivyo akipokea mpira pale pale anajua shimo liko wapi....ndiyo maana hapotezi mpira hovyo.
Kwa bahati nzuri Mungu kamjalia ujuzi wa hali juu hivyo zile chenga za mwili (body faints) kwake zimejaa...ndiyo maana anaweza kufanya half-turn za kutosha kati kati ya msitu wa watu.
Akiwa kwenye Zone 14 ni mtu hatari sana kwani ana jicho la kupiga pasi chonganishi kwenye half-space (kati kati ya Fullback na Center-back) hivyo winga wake au Fullback wanakutana nazo kwenye box na kufanya mambo yatokee.
Halafu mbaya zaidi jamaa ana engine kubwa ya ku-press.
Ubongo,Ubongo,Ubongo,Ubongo......Pacome ni Ubongo mtupu