Ukiambiwa Wizara ya raha imehamia Yanga katika nyanja ya Soka usikatae hata kidogo.
Hiyo ni baada ya Yanga kukamlisha usajili wa Winga kutoka Marumo Gallants ya Afrika ya Kusini, Mahlatse Makudubela maarufu kama "Skudu".
Skudu ana uwezo wa hali ya juu kucheza na mpira na kutoa burudani kwa Mashabiki wanaopenda "tuvitu vitu" Uwanjani.
Tanzaniaweb tumekuletea mkusanyiko wa Clip za Mchezaji huyo akiwatoa jasho mabeki wa Timu pinzani.
Kwa mara ya kwanza Skudu ataonekana leo dhidi ya Kaizer Chiefs katika kilele cha Siku ya Mwananchi Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Tazama vitu vya Skudu kwenye Video hapa chini halafu utupe Comment yako kuelekea msimu ujao;