Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba wamuaga Mkude kwa Mkapa

Jonasmkude20 Jonas Mkude

Sun, 6 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo aliyeitumikia Simba kwa miaka 13 Jonas Mkude ameagwa kwa kupigiwa makofi kwenye tamasha la Simba Day.

Mkude sasa anakipiga Yanga baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia timu hiyo yenye maskani yake Jangwani.

Mkude ametupiwa vilago na Simba dirisha hili la usajili baada ya mkataba wake kumalizika na jezi yake namba 20 aliyokuwa akiivaa alipokuwa Simba amekabidhiwa beki wa kati wa kimataifa Che Malone.

Pamoja na kutokuwepo kwenye tamasha hilo kutokana na kuwa kambini kwenye timu yake mpya mashabiki wa Simba waliombwa kusimama na kumpigia makofi kutokana na kuitumikia timu hiyo kwa muda mrefu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: