Ndani ya saa 3 tu tokea jezi yao mpya ya msimu wa 2023/24 kuwekwa mtandaoni, mashabiki Simba wameandika REKODI ya kugonga LIKES zaidi ya LAKI MOJA.
Sasa Simba wanafuatiwa na watani wao Yanga ambao jezi yao mpya ya 2023/24 ilitangazwa Julai 7, tofauti ya siku 14 au wiki mbili na hadi sasa ina LIKES 24,000 na ushee...wakiwa nyuma MARA NNE dhidi ya watani wao hao ambao hawajafikisha hata robo siku.
Page ya Simba ina wafuasi milioni 5 Yanga wafuasi milioni 2.6.
Wengine waliozindua jezi msimu huu ni Azam FC na Singida Fontaine ambao hata hivyo kurasa zao bado hazina nguvu kama vigogo hao wa Kariakoo.