Wakati Singida Fountain gate wakijiandaa kushuka Dimbani leo Jioni kumenyana dhidi ya Simba SC katika Uwanja wa Mkwakwani.
Singida Fountain Gate itakosa huduma ya Wachezaji wake wawili ambao wanaitumikia klab hiyo kwa mkopo
Joash Onyango
Habib kyombo
Huku Simba SC nayo itakosa Huduma ya Viungo wake wawili ambao wanatumikia adhabu ya kadi na kufungiwa
Sadio kanoute
Clatous Chama
SIMBA SC NI MBABE WA SINGIDA FOUNTAIN GATE
Takwimu za michezo waliyokutana Singida Fountain gates na Simba SC ni dhahiri Simba ni mbabe wa Walima alizeti.
Katika historia wamekutana Mara mbili tu na wametoa sare moja na Simba ameshinda mchezo mmoja huku Singida wakiwa hawajapata ushindi.
Kwenye michezo hiyo miwili baina ya miamba hao wawili, yamefungwa jumla ya mabao sita.
Mabao manne kati ya hayo amefungwa Singida na mawili amefungwa Simba SC
Leo wanakutana kwenye nusu fainali ya pili ya Ngao ya Jamii huku timu zote zikiwa zimefanya usajili wa kibabe kwa ajili ya mashindano mbalimbali ambayo wanashiriki.