Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba SC yawabana Onyango, Kyombo

Onyango Singida FG Simba SC yawabana Onyango, Kyombo

Thu, 10 Aug 2023 Chanzo: Dar24

Beki kutoka Kenya Joash Onyango na Mshambuliaji Mtanzania Habib Kyombo hawatakuwa sehemu ya kikosi cha Singida Fountain Gate kitakachoikabili Simba SC.

Wawili hao wanaocheza kwa Mkopo Singida Fountain Gate wakitokea Simba SC, wanabanwa na makubaliano yaliyofikiwa kimkataba baina ya pande hizo mbili.

Ikumbukwe kuwa Singida Fountain Gate itacheza na Simba SC leo Alhamis (Agosti 10) katika Nusu Fainali ya Pili ya Ngao ya Jamii, Uwanja wa CCM Mkwakani jijini Tanga.

Mshindi wa mchezo huo atacheza dhidi ya Young Africans iliyotangulia Fainali baada ya kuigunga Azam FC jana Jumatano (Agosti 09), Uwanjani hapo.

Chanzo: Dar24
Related Articles: