Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sadio Kanoute amepewa "Thank you" Simba SC?

Simba Wamtema KANOUTE Abdallah Hamis ndie mchezaji alievaa jezi namba 13, ambayo huvaliwa na Kanoute

Fri, 28 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wakati mjadala ukiwa ni jezi namba 20 katika klabu ya Simba ambayo hapo awali ilisemekana kwamba itastaafishwa kwa heshima ya kiungo wake Jonas Mkude na jana katika mchezo wa kirafiki kuonekana imevaliwa na mchezaji mwingine.

Wengi wameikosoa Klabu ya Simba kwa kitendo hicho huku ikionekana kama ni maamuzi ya kutomheshimu Mkude kwa makusudi hasa baada ya kuonekana amejiunga na watani zao Klabu ya Yanga.

Sasa kuna jipya ambalo pengine wengi bado hajaligundua katika michezo miwili ya kirafiki waliyocheza Simba SC jana Julai 27.

Jezi namba 13 ambayo huvaliwa na kiungo wake raia wa Mali Sadio Kanoute "Putin" nayo alipewa mchezaji mpya aliesajiliwa dirisha hili Abdallah Hamis.

Kitendo hicho kimeibua maswali kwa wengi wakihoji je Sadio Kanoute amechwa? ikizingatiwa kuwa Simba imezidisha idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kuwa nao 12 na sasa ina wachezaji 13.

Je Sadio Kanoute ameachwa na Simba ili kukamilisha idadi ya wachezaji 12 wa kigeni wanatakiwa kikanuni?

Kama hajaachwa kitendo cha mchezaji mwingine kupewa jezi yenye namba ya Kanoute kina maana gani?

Tupe maoni yako kwa kutuandikia katika kisanduku cha maoni na utueleze unalionaje suala hili

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: