Thu, 24 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tetesi kutoka ndani ya Simba Sc zinaeleza kuwa kocha mkuu wa timu hiyo Robertinho ameutaka uongozi wa timu hiyo kuwafyeka wachezaji watatu ambao wameshindwa kuonyesha uwezo ndani ya timu hiyo.
Kocha huyo ameutaka uongozi wa timu hiyo kuwatoa wachezaji hao kwa mkopo ili kwenda kuonyesha uwezo wao tofauti na kuishia bechi ndani ya Simba.
Taarifa zinaeleza kuwa wachezaji ambao watatolewa kwa mkopo baada ya kushindwa kuonyesha uwezo mzuri ni pamoja na Jimyson Mwinuke, Ahmed Feruz na Mohammed Mussa watatolewa kwa mkopo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: