Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amenunua tiketi 5000 kuelekea mchezo wa fainali ya kombe la shirikisho Afrika kati ya Yanga na USM Algers utakaopigwa Mei 28 katika dimba la Benjamini Mkapa.
Akiwasilisha ahadi hiyo ya Rais Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa amesema lengo la Rais Samia ni kutengeneza mazingira mazuri kwa Yanga kutwaa ubingwa wa shirikisho Afrika na kuandika historia mpya kwenye soka la Tanzania.
Aidha Msigwa amesema Rais Samia amewataka wadau wengine kujitokeza kununua tiketi kwa ajili ya mchezo huo ili kuwapa nafasi mashabiki wengi zaidi kuhudhuria mchezo huo na Yanga kuutumia vyema uwanja wa nyumbani kwa nguvu ya mashabiki.