Meneja habari wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa, Swaleh Suleiman yuko tayari kununua Kibegi ama Jezi itakayozinduliwa Ijumaa kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro kwa milioni mbili.
“Swaleh Suleiman Madjapa (Mwenye Miwani) yuko tayari kununua Kibegi au Jezi itakayozinduliwa juu Mlima Kilimanjaro kwa Shilingi Milioni 2.”- Ahmed Ally
Mtoto huyo wa Mzee Ally ameongeza kuwa; “Simba tumetangaza kuziuza Jezi zote 6 zitakazozinduliwa Juu ya Mlima Kilimanjaro kwa njia ya mnada.
“Fedha zitakazopatikana kutoka kwenye mnada huo zitapelekwa kwenye ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto katika Hospital ya Muhimbili.”