Aliyekuwa winga wa Yanga SC, Bernard Morrison amemwagia sifa kedekede winga mpya wa klabu hiyo, Mahlatse Makudubela almaarufu Skudu' akidai amejifunza mengi kutoka kwake na kuongeza kuwa yeye ni shabiki wake namba moja.
Aliyekuwa winga wa Yanga SC, Bernard Morrison amemwagia sifa kedekede winga mpya wa klabu hiyo, Mahlatse Makudubela almaarufu Skudu' akidai amejifunza mengi kutoka kwake na kuongeza kuwa yeye ni shabiki wake namba moja. "Ni furaha ilioje... hakuna haja ya kuzungumza mengi kwa sasa. Baadae nitazungumzia jinsi ninavyojivunia kukuleta hapa. Nenda ioneshe Tanzania kile ulichonifundisha. Mimi ni shabiki wako namba 1. NAKUPENDA KIJANA WANGU." ameandika Morrison kwenye ukurasa wake wa mitandao ya kijamii.