Mon, 14 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkurugenzi wa Ufundi wa Simba, Juma Mgunda, inaelezwa sasa amepewa jukumu jipya la kuiongoza Simba Queens, akichukua mikoba iliyoachwa na Mganda, Charles Lukula.
“Ni kweli kwa sasa kikosi cha timu ya wanawake amekabidhiwa majukumu Mgunda, atakuwa akifundisha timu hiyo huku makiendelea na majukumu yake mengine ya ufundi kwa timu zote za Simba,” kilisema chanzo kutoka ndani ya Simba
Mpaka sasa Kikosi cha Simba Queens kimeshusha mashine tatu mpya; Isabelle Diakiese kutoka Bikira FC ya DRC, Ritticia Nabbosa wa Fountain Gate na Joanitha Ainembabazi aliyekuwa Ceasiaa Queens.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: