Wananchi bado hawajakata tamaa licha ya kupoteza mchezo wa mkondo wa kwanza wa Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Meneja wa Klabu ya Yanga Walter Harisson amesema wanakwenda katika mchezo huo wakiwa wamebeba matumaini ya Taifa. Na wanafanya mazoezi kila siku kurekebisha makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa kwanza.
“Tunaendelea na mazoezi na Inshallah siku ya Alhamis Mwenyezi Mungu akijalia tutaanza safari ya kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa marudiano.
“Tuko tayari kuhakikisha tunaenda kuitetea Bendera ya wananchi tuko tayari kuitetea bendereza ya nchi,” Meneja wa Yanga Sc, Walter Harrison