Sun, 28 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baadhi ya mashabiki wa Yanga imewabidi kupanda uzio wa uwanja ili kuingia ndani kuishuhudia timu yao ikicheza fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger.
Ni kama watu wa usalama wanaonekana kuzidiwa na mashabiki hao kwani wamekuwa wakiwategea kisha kufanya jaribio la kuingia uwanjani kwa njia zisizo rasmi.
Kila ambapo watu wa usalama walipokuwa wakiwazuia geti moja walikimbilia lingine na kuingia. Hata hivyo wapo ambao waliruka ukuta na kukumbana na vizuizi vingine lakini asilimia kubwa walipenya na kuungana na wale ambao walikuwa kwenye utaratibu na kuingia uwanjani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: