Kocha wa Makipa wa Ihefu, Peter Manyika amesema ili timu zetu zifanye vizuri kimataifa inatakiwa maandalizi bora kwa maana ya kupata wachezaji sahihi watakaoweza kufanikisha malengo hayo.
"Nimefanya kazi katika bara la Afrika na nje ya Afrika hivyo kuna vitu nimeviona ambavyo vinaweza vikatusaidia, kipindi chetu tulikuwa tunapata michezo mikubwa kabla ya mashindano yenyewe kitu ambacho kilikuwa kinawafanya wachezaji kutengeneza ile hali ya kujiamini zaidi."
Manyika ametoa maoni hayo wakati akichangia mada iliyoandaliwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited kwenye mtandano wa kijamii wa X Space iliyokuwa inaeleza nini kifanyike klabu za Tanzania zifanye vizuri kimataifa.