Thu, 20 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Msemaji wa Klabu ya Yanga, Haji Manara ameeleza kuwa timu hiyo haiwezi kumzuia Fiston Mayele kuondoka iwapo ikitokea klabu kubwa imeweka fedha ya kutosha kumsajili na yeye akaridhia.
"Yanga haiwezi kumzuia Mayele Fiston kuondoka iwapo ikitokea Club imeweka mzigo wa kutosha na yeye mwenyewe akiridhia kutaka kuuzwa, muhimu ikitokea hivyo Washabiki lazma tuunge mkono maamuzi hayo.
"Yes, Football ipo hivyo na tusisahau football ya sasa ni biashara kamili kama kuuza ndizi au dhahabu tu," ameandika Haji Manara kwenye Ukurasa wake wa Instagram.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: