Wakati wengiwakiona kama vile usajili wa Kiubgo Jonas Mkude katika Klabu ya Yanga hauna maana wala faida kwa Yanga bali ni kumkomoa mtani ukizingatia Yanga imesheni utajiri wa Viungo wa kati.
Basi hiki ndicho kilichompeleka Jonas Mkude kwa matajiri wa Jangwa Young Africans SC.
Jonas Mkude anaenda kuwapa Yanga wasifu ama 'profile' ya namba 6 ambaye pale Yanga walikuwa na uhaba naye. Kwa maana ya Holding/Deep lying ambayo alikuwa anaioffer Khalid Aucho peke yake.
Zawadi Mauya, Yannick Bangala, Sureboy na Mudathir Yahya hawana wasifu wa kuchezesha timu kutokea chini.
Ndio maana alipokuwa anakosena Aucho msimu uliopita, pengo lake lilikuwa linaonekana licha ya timu kuwa na 'namba 6' wengine takribani 4. Mkude anakwenda kuwapa uhakika wa maisha bila ya Aucho msimu ujao.