Mchezaji anapokuwa na umri mkubwa kwenye soka na anajua anahitajika na klabu ni lazima atake maboresho ya maslahi, kwake huwa ndio kama anayaandaa mafao yake ya kustaafia.
Ni kama ambavyo klabu huwa inamtaka mchezaji mwenye umri mkubwa apunguze mshahara ili abakie kama klabu inakuwa na hiari juu yake kutokana na ushindani uliopo kwenye nafasi yake. Mtu yeyote angefanya kama alivyofanya Chama Jr.
Modric akiwa na miaka 32 mwaka 2018 kama ilivyo Chama hivi sasa aliboreshewa maslahi lakini miaka 3 baadae walipokaa tena mezani na Real Madrid huku tayari Fede Valverde akionekana yupo tayari kukaimu vizuri tu nafasi yake ikabidi apunguze mshahara ili aweze kusalia klabuni hapo.