Mon, 14 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakati Yanga wakipoteza Kombe la Ngao ya Jamii kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha miaka miwili kwa kupoteza mchezo wa Fainali jana Agosti 13 mbele ya Simba SC.
Aliekuwa shujaa wa Timu hiyo mbele ya Simba Fiston Mayele ambae kwa sasa amejiunga na FC Pyramids ya misri amewapa pole waajiri wake wa zamani na kuwataka waangalie zaidi Ligi.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mayele ameandika
"Jana imepita, muangalie Ligi sasa Inshallah"
Mayele kwa miaka miwili mfululizo aliwapa Yanga ushindi mbele ya Simba katika mchezo wa Fainali ya Ngao ya Jamii 2021 na mwaka 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: