Kocha Msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze aipongeza klabu hio kwa kujituma na kudhihirisha ukakamavu uliohusisha utimiaji mzuri wa fursa za makosa yalioonekana kwa wapinzani wao katika Michuano ya kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Jitihada hizo walizoonyesha zimeweza kuwapatia ushindi dhidi ya TP Mazembe ikiwa ni miongoni ya timu kubwa barani Afrika.
“Pongezi kubwa kwa vijana wetu, wameonyesha ukomavu katika mchezo mgumu kwenye mazingira magumu dhidi ya moja ya Klabu kubwa barani Afrika, tunashukuru kwa sapoti kubwa kwa Mashabiki wetu na Uongozi kwa ujumla. Wananchi furaha yenu ndio fahari yetu,” amesema Cedric Kaze.