Michezo ya Ngao ya Jamii 2023 imekamilika Agosti 13 Mwaka huu kwa Fainali ambayo iliwakutanisha vigogo Simba na Yanga katika Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Simba waliibuka wababe kwa kunyakua ndoo hiyo kwa Mikwaju ya Penati mbele ya Yanga waliokuwa wamebeba Kombe hilo mara mbili mfululizo.
Sasa Mchambuzi wa Michezo nchini kutoka EFM, Jemedari Said amesemema mchezo unapozikutanisha timu hizo mbili huvuta hisia za wengi na hata kibiashara timu hizo zina mvuto.
Sasa Jemedari amehoji namna mamapato yaliyopatikana katika mashindano ya mwaka huu na namna mgao ulivyotolewa.
Msikilize Jemedari Said hapa chini;