Thu, 1 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino ameipongeza Yanga SC kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2022/2023.
Katika pongezei hizo, Infantino amesema isingekuwa rahisi kutwaa ubingwa huo bila bidii ya timu nzima, ari na kujitolea na kila mtu kwenye timu hiyo anajivunia hilo.
Aidha, amelipongeza Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa mchango wake katika maendeleo ya soka nchini Tanzania na Afrika.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: