Fri, 21 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba SC leo Julai 21 imezindua Jezi zake za msimu mpya 2023/24 katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Sasa tangu Jumatano kibegi kilianza safari ya kuelekea katika kilele cha Mlima Kilimanjaro na leo Ijumaa kiliwasili na kilibeba jezi mpya tano zikiwa na majina ya Viongozi wa Serikali na moja ikiwa na jina la Rais wa Heshima wa Simba Mohammed Dewji.
Majina ya viongozi hao ni Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi na Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: