Ligi Kuu Bara imemalizika wiki mbili zilizopita na kushuhudiwa Yanga ikitetea taji kabla ya kubeba pia Kombe la ASFC, lakini kwa sasa mashabiki wanapata burudani nyingine kutokana na kuwepo kwa kaligi flani matata ya wachezaji na makocha wanaotemwa na kuagwa na timu kwa 'Thank You'.
Azam FC ndio iliyoanza kwa kutangaza kuwatema makocha wake kabla ya kugeukia wachezaji kisha kufuatiwa na Yanga na Simba, lakini kabla ya thank you za jana, Wanalambalamba walikuwa wakiongoza msimamo wa kugawa 'thank you' nyingi.
Mwanaspoti kupitia thank you hizo zilizotolewa hadi sasa, imetengeneza kikosi kabambe cha wachezaji waliotemwa na makocha hao, sambamba na msimamo wa kaligi hako kalivyo kwa sasa;
Kikosi kilivyo:
Mahmoud Mroivili, Emiry Nimubona, Bruce Kangwa, Joseph Zziwa, Mohamed Ouattara, Victor Akpan, Tuisila Kisinda, Cleophas Mkandala, Rodger Kola, Bernard Morrison na Augustine Okrah
Akiba: Wilbol Maseke, Kenneth Muguna, Dickson Ambundo, Nelson Okwa, Geurold Mwamba wa Mwamba na Djibril Olatunje, Gadiel Michael
Kocha: Fred Felix 'Minziro' na Kally Ongala
Msimamo wa Ligi wa 'Thank You'
1. Simba SC (12)
2. Azam FC (10)
3. Coastal (7)
4. Namungo (7)
5. Yanga SC (6)
6. KMC FC (1)
7. Geita Gold (1)