Simba jana ilicheza mechi ya Fainali ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga kwatika Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa Penati 3-1.
Tofauti na matarajio ya wengi, katika kikosi kilichoanza jana nyota Kibu Denis ambae amejihakikishia kuanza katika kikosi cha Robertinho jana alianzia benchi huku winga, Jose Luis Miquissone akipata nafasi ya kuanza.
Pengine wengi walipata wasiwasi kwa kuwa Miquissone bado hajaonesha fomu yake tangu atue Simba siku chache zilizopita sasa Mchambuzi wa Michezo kutoka EFM, Geof Lea ametoa hoja zake kwanini ilikuwa ni muhimu kwa Miquissone kuanza nafasi ya Kibu.
Msikilize Geof katika Video hapa chini;