Kocha Mkuu wa Yanga, Miguel Gamondi amesema mechi tatu mfululizo walizozipata zimeongeza ufiti kwa mastaa wake huku akilia na mapumziko yaliyo mbele yao kwamba yanashusha morali ya wachezaji.
“Kikosi changu kipo imara sina wasiwasi na mchezo huo nimewaandaa kwaajili ya kushindana na wamekuwa wakifanya kile ninachowaelekeza; Tunahitaji matokeo kwenye kila mchezo ulio mbele yetu.”
“Mapumziko marefu yanaweza kupelekea kuanza upya kutokana na sifa za wachezaji kutokuwa pamoja ndani ya muda kunavyowafanya kujiweka fiti upya. Wachezaji ni kama watoto wasipoelekezwa nini wafanye wanajiachia na kufanya mambo ambayo kisoka ni lazima waanze moja.”