Uongozi wa Fountain Gate Princess kupitia kwa Ofisa Habari wao, Kuruthum Hassan umefunguka kuwa lazima watoe unyonge na kupata alama tatu mbele ya Simba Queens kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Wanawake Bara.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Aprili 5, katika Uwanja wa Fountain, uliopo mkoani Dodoma.
Kuruthum amefunguka kuwa: “Kikosi kinaendelea na maandalizi kwa ajili ya mchezo huu ambao ni muhimu sana kwetu kupata ushindi kwa sababu kwenye mashindano yote ya ligi hatukuwahi kupata ushindi mbele ya Simba Queens.
“Safari hii tunahitaji alama tatu kwa namna yoyote ile, haiwezekani tuweze kumfunga mtani wake Yanga zaidi ya mara moja halafu tushindwe kumfunga yeye.”