Baada ya kufanya makubwa msimu uliopita akiwa na kikosi cha Yanga nyota mpya wa kikosi cha Pyramids amechaguliwa kuwa mchezaji bora anayeendelea Afrika kwa kupata kura 140,000
Mayele amewashinda Mahmoud Kahraba na Khaled Bousseliou, Mayele amekuwa na msimu mzuri 2022/23.
Kura hizo zimepigwa na tovuti inayojihusisha na masuala ya soka Afrika ijulikanayo kama Foot_Afrika.
Katika Mashindano aliyoshiriki msimu wa 2022/23.
Magoli 7 Kombe la Shirikisho Afrika.
Magoli 17 Ligi kuu Tanzania Bara.
Magoli 7 Ligi ya Mabingwa Afrika( hatua ya awali).
Magoli 2 Kombe la FA.
Una neno lipi la Kumzungumzia Fiston Mayele? Tupe maoni yako