Thu, 1 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kitendo cha Mchezaji wa Yanga Feisal Salum kukaa pasipo kucheza mpira hata yeye hakipendi kwa kuwa yeye ni mtoto wa Kimasikini na ili apate kipato lazima acheze mpira.
Mbali na hilo Mchezaji huyo amedai mzazi wake ni mgonjwa na yeye ndio anasimamia matibabu hivyo pasipo kupata pesa kupitia kucheza mpira kwake inakua shida.
“Mimi nimetokea kwenye familia ya kimasikini, mimi nasaidia familia yangu, ili mambo yaende ni lazima mimi nifanye kazi, Baba yangu anaumwa na mimi ndio nasimamia matibabu, yeye mwenyewe hapendi hili sakata liendelee kwasababu kuna mambo yanakwama"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: