Mon, 5 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz, ametimiza ahadi yake kwa golikipa wa Yanga, Djigui Diarra, kwa kumkabidhi Dola za Kimarekani 4200 zaidi ya shilingi milioni 10 za Tanzania.
Diamond alitoa ahadi hiyo Juni 3 baada ya Mlinda mlango huyo wa Yanga kuonesha kiwango safi katika mchezo wa mkondo wa pili wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Algiers.
Katika mchezo huo wa Fainali Diarra aliokoa mkwaju wa Penati na pia aliibuka nyota wa mchezo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: