Mshambuliaji kutoka Yanga Princess na Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Clara Luvanga (18) amefanikiwa kujiunga na Klabu ya Dux Logronoinayoshiriki ligi daraja la kwanza (wanawake) nchini Hispania.
Clara ambaye amefanya makubwa kwenye soka la wananwake nchini amesaini mkataba wa miaka mitatu (3) akitokea Yanga Princess inayoshiriki Ligi Kuu ya wanawake Tanzania.
Kwa rekodi ya miaka 10 ya hivi karibuni, Clara Luvanga anakuwa mchezaji wa kwanza wa kike kucheza soka la kulipwa nchini Hispania na pia waajiri wake wa zamani Yanga Princess wanaweka rekodi ya kumuuza mchezaji wao huyo katika moja ya Ligi kubwa Barani Ulaya.