Viungo wa Simba SC, Clatous Chama na Fabrice ngoma wamewasili katika Kambi ya Simba iliyopo nchini Uturuki kuungana na wenzao kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.
Simba wameweka Kambi ya Kujiandaa na msimu ujao 2023/24 nchini Uturuki na watakaa humo kwa muda wa wiki tatu.
Kubwa lililowavutia Wanasimba ni kuona kiungo wao kipenzi Chama akiungana na Timu baada ya kutokea sintofahamu baina yake na Klabu siku kadhaa zilizopita.
Tazama Video hapa chini mastaa hao wakiwasili Kambini;
Hivi ndivyo Clatous Chama na Fabrice Ngoma walivyowasili kambini usiku huu hapa nchini Uturuki. #NguvuMoja pic.twitter.com/U8eN9ARwrL
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) July 20, 2023
Je umeipokeaje taarifa ya Chama kujiunga na Kambi? Tuachie maoni yako