Baada ya kufuzu hatua ya robo fainali Kombe la Shirikisho Afrika, Yanga imesafiri kwenda Nigeria kucheza mchezo wa kwanza wa hatua hiyo dhidi ya Rivers United utakaochezwa tarehe 23 siku ya Jumapili.
Kikosi kikiwa kimesafiri, maandalizi ya mchezo wa marudiano yameshaanza na hapo jana Afisa Habari wa klabu, Ally Kamwe alitangaza viingilio vya mchezo huo utakaochezwa tarehe 30 kwenye dimba la Benjamin Mkapa majira ya saa 1 usiku.
“Tiketi za mchezo wetu wa marudiano dhidi ya Rivers United utakaochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa tarehe 30.04.2023 zitaanza kuuzwa leo.
"Na mimi kama Afisa habari wa Klabu yetu nitajivunia sana kuona tunabadili utamaduni na kununua tiketi mapema hii itakwenda kuongeza morali kubwa kwa wachezaji wetu kwenye maandalizi ya mchezo huu wa kihistoria,” alisema Ally Kamwe.
Viingilio hivo ni kama ifuatavyo;